Previous
Next

Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Kilimo kwa Mwaka 2025/2026 ya shilingi trilion 1.24 tarehe 21 Mei, 2025, Bungeni jijini Dodoma. Pamoja na viongozi wengine waliohudhuria wasilisho hilo ni Mhe. David Silinde (Mb), Naibu Waziri wa Kilimo, menejiment ya Wizara ya Kilimo pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TOSCI, ndugu Nyasebwa Chimagu.

Wafanyakazi wa Wizara ya Kilimo na taasisi zake wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe (Mb), Naibu Katibu Mkuu Dkt. Hussein M. Omar, Mkurugenzi Mkuu wa TOSCI Ndg Nyasebwa Chimagu, Mkurugenzi Mtendaji wa TASTA Ndg Bob Shuma na mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya bunge ya viwanda, biashara, kilimo na mifugo

Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe (Mb), akihutubia wawakilishi wa makampuni ya mbegu (hawapo kwenye picha) waliohudhuria mkutano wa mwaka wa wadau wa mbegu uliofanyika tarehe 15 Mei, 2025 jijini Dodoma katika hoteli ya Midland Inn.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) ndugu Nyasebwa Chimagu, akihutubia wawakilishi wa makampuni ya mbegu (hawapo kwenye picha) waliohudhuria mkutano wa mwaka wa wadau wa mbegu uliofanyika tarehe 15 Mei, 2025 jijini Dodoma katika hoteli ya Midland Inn.

Baadhi ya wawakilishi wa Makampuni ya mbegu waliohudhuria Mkutano wa taifa wa wadau wa tasnia ya mbegu nchini uliofanyika tarehe 15 Mei, 2025 jijini Dodoma katika hoteli ya Midland Inn.

Picha ya pamoja ya wajumbe wa BODI ya Wakurugenzi ya TOSCI na Menejimenti ya TOSCI baada ya kumalizika kwa kikao cha BODI kilichofanyika mkoani Njombe tarehe 02/07/2023

Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa TOSCI na Naibu Waziri wa Kilimo Mh. David Silinde (Mb), siku alipotembelea Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania

-

-
